Propellerads
Propellerads
Propellerads
Daily Updates!

We share informations with you

Propellerads

Saturday, 18 February 2017

ADAM BARROW SWORN ONCE AGAIN IN GAMBIA



The Gambia has sworn in its new president, Adama Barrow, in front of a crowd of thousands.
It is the second time Mr Barrow has taken the oath.

The first time was at very low-key event at the country's embassy in Senegal last month, after a lengthy power struggle forced him into exile.
After his predecessor finally agreed to step down, Mr Barrow was able to arrange a stadium event back in his homeland, near the capital city Banjul.

Crowds queued through the night to get a good spot inside the stadium.
Brass bands prepared to play and flags waved.
Mr Barrow is only the third president in the history of The Gambia, and the celebrations also mark 52 years of the west African country's independence.


Long-time leader Yahya Jammeh was voted out in December but he only agreed to step aside when regional powers sent in troops ready to remove him by force.
He has since fled to Equatorial Guinea.


Mr Barrow has promised a new dawn for the country, which Mr Jammeh had ruled with an iron fist.
Many political prisoners have already been freed and The Gambia is set to rejoin international institutions such as the International Criminal Court and the Commonwealth.

Mr Barrow, a successful property developer who has never held public office, defied the odds by winning the election.


EVEN A DEAD MUGABE WILL BE A ZIMBABWE PRESIDENT



The wife of Zimbabwe's 92-year-old President, Robert Mugabe, has said that he is so popular that if he died, he could run as a corpse in next year's election and still win votes.
Grace Mugabe, 51, was addressing a rally of the governing Zanu-PF party.
Mr Mugabe has governed Zimbabwe since the end of white-majority rule in 1980 following a bitterly fought war.

His wife, who has often professed her undying loyalty to her husband, has assumed an increasingly high profile.
"One day when God decides that Mugabe dies, we will have his corpse appear as a candidate on the ballot paper," Mrs Mugabe told the rally in Buhera, south-east of the capital Harare.

"You will see people voting for Mugabe as a corpse. I am seriously telling you - just to show people how people love their president."
President Mugabe has been backed by his party to stand again in next year's election, but recently cut back on his public engagements.

Grace Mugabe has warned contemporaries of Mr Mugabe from the guerrilla war era that they are not in a position to replace him because they likewise would be too old.
"Anyone who was with Mugabe in 1980 has no right to tell him he is old. If you want Mugabe to go, then you leave together. You also have to leave. Then we take over because we were not there in 1980," she said, gesticulating towards herself.



Last September, the president was rumoured to have died after he reportedly cut short his attendance of an AU summit to fly to Dubai for a health check.
Mr Mugabe later joked about the rumours, saying he indeed died but was only resurrected

MAMELOD SUNDOWNS WINS SUPER CUP CROWN


Mamelodi Sundowns picked up yet another piece of silverware after they defeated DR Congo giants TP Mazembe 1-0 at Loftus Versfeld to claim the CAF Super Cup on Saturday evening.

The Brazilians were victorious in the annual exhibition match thanks to a late penalty from Ricardo Nascimento. It was a deserved triumph for the South African champions, who dominated the vast majority of the match.

The first clear chance of the encounter went the way of Mazembe, with striker Ben Malango sprinting free on goal in the ninth minute. He beat Denis Onyango with his first shot, but the ball crashed into the upright.

The Mazembe striker got onto the rebound and looked sure to score with a second attempt, but Onyango recovered well to push the effort onto the same post and deny the DRC giants an early lead.

Sundowns generally enjoyed the majority of ball possession in the first half, but it was only in the final minutes before the break that they really looked like capitalising on their dominance.

Khama Billiat should have at least hit the target when presented with a clear sight of goal in the 37th minute, while Anthony Laffor almost snuck a shot into the bottom corner just before the break, but goalkeeper Sylvain Gbohouo did just enough to keep it out.

From the start of the second half, the Brazilians were even more dominant and created a string of openings from which they should have broken the deadlock. However, the likes of Hlompho Kekana, Laffor and Tiyani Mabunda were all guilty of spurning good opportunities.

It seemed only a matter of time until ‘Downs broke through and the Ravens’ defence finally cracked with just under 10 minutes to play, as Kekana was clumsily brought down in the box to win a penalty. Defender Ricardo Nascimento coolly converted from the spot to claim the game’s decisive goal in the 83rd minute.

A PLAN TO END EARLY MARRIAGE IN TANZANIA


A five-year plan has been adopted by Plan International organization to prevent over 12,000 young girls in four regions in Tanzania from child marriage.

The regions include Mara, Rukwa, Geita and Morogoro which will benefit through educational and economic empowerment of girls and women. According to Plan International country coordinator, Mr Jorgen Haldorsen.

He told a news conference that the plan, which is under a global strategy to eliminate gender discrimination, aims at reaching out to over 100 million women and girls who are vulnerable to gender violence worldwide.

“The move in the regions will target the elimination of child marriage and gender based violence by helping women learn about gender issues, participate in socio-economic and political decision, have control over their lives and bodies and finally protect themselves from discrimination, violence and fear,” he explained.

The 2016 Tanzania Demographic Health Survey showed that 33 per cent of Tanzanian girls experience sexual violence before the age of 18 while two out of five girls are married before attaining 18 years.

REFUGEE CHILDREN TO ATTEMPT EXAMS UNDER NECTA


Speaking with journalists shortly after winding up a two-day Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern Africa; Education, Science and Technology Minister, Prof Joyce Ndalichako, said Tanzania for many years adhered on human rights including the right to education not only to its citizens but also to refugees.

“We agreed that education for all which is implemented in our countries and by all people - refugees are also included as long as they are within our countries.

They have the right to education. It is true that Tanzania has been home for many refugees. We are adhering to human rights, education being one of them. We are finalising preparations of examinations for Burundi children who are living in refugee camps.

We follow their national curriculum,” the minister said. The move was applauded by a number of international agencies and human right watch bodies. Among the topics that were debated by various education stakeholders was inclusion of displaced children in educational programmes.

Prof Ndalichako, who doubled as chairperson of the forum, said in order to improve the quality of education in the region, the highlevel government representatives agreed to improve teachers’ welfare. They also agreed to carry out campaigns to boost enrolment of disadvantaged and most vulnerable children and those with disabilities.

Other agreements included taking measures to address data gaps, monitoring the situation of outof- school children and youths and the inclusion of refugee education, strengthening early learning. They also opted to recognise the importance of gender equality and women’s empowerment, initiate policy and curricula reforms to rebrand and revive Technical- Vocational Education and Training (TVET).

“The government is determined to work closely with other stakeholders to attain quality and inclusive education as well as equitable and life-learning for all children, youths, men and women, regardless of their circumstances or backgrounds,” she said.

YANGA SCORED 1:1 ANGAIST NGAYA FC FROM COMORO

Yanga has succeeded in moving ahead in the first round of the African Champions League despite getting a 1-1 draw against the Comoro Ngaya Club at the National Stadium in Dar, Saturday.


The teams are from the draw in the game, which was no great pressure to have the original game Yanga won 5-1 in the Comoros.


In a game played Nation, Comoros those who are the first to get a goal early in the first period, before Yanga Mwinyi Haji equalizer through in the 43rd minute.


In the game players Yanga had several clear chances but failed to use them properly, Obrey Chirwa missed a goal in minute 48 and 51, Emmanuel Martin and he was unable to use the open space and 56 minutes.


Due to the inability to use the space he had, Yanga coach, George Lwandamina Martine decided to cast off and replaced by Juma Mahadhi who also had a chance 61 minutes he was unable to use it properly.


Yanga made other changes to betraying Hassan Juma Abdul and enter Kessy 71st, Deus Kaseka he went out 81 minutes and incorporate Said Juma basket.

BINADAMU KUTUMIA MOYO WA PLASTIKI

NCHINI Marekani kila baada ya dakika 10 mtu mmoja huwekwa kwenye foleni ya watu wanaosubiri kuwekewa moyo mpya ili kuweza kuendelea kuishi. Hali hii hotokea baada ya moyo wa mgonjwa kuonekana hauwezi kufanyiwa matibabu na hivyo njia pekee ya kuokoa maisha yake ni kupata moyo mpya ambao huwekewa kwa njia ya upasuaji (transplant).

Shirika la Umoja wa Kuchangia Viungo, linasema kuwa takribani watu 22 hufariki dunia kila siku nchini Marekani wakiwa katika foleni ya kusubiri mtu wa kujitolea moyo kwa ajili ya kuokoa maisha yao. Hata hivyo, wagonjwa wa aina hii sasa wanaweza kufurahia baada ya ugunduzi wa moyo wa bandia ambao inawezekana wakautumia kwa maisha yao yote (Total Artificial Heart)TAH).

Mtu anayechangia moyo (donor) anaweza kuwa ni mtu ambaye tayari ubongo wake umekufa lakini mwili bado una uhai na hivyo moyo wake kuwa mzima. Mgonjwa wa aina hii hawezi kupona. Mgonjwa yeyote ambaye ana hali mbaya lakini ugonjwa wake hauhusiani na moyo na ambaye hawezi kupona pia anaweza kujitolea moyo. Mtu aliyefariki pia anaweza kutolewa moyo na kusaidia wenye uhitaji lakini mara nyingi hii huwa ni kwa ridhaa yake kabla hajafariki.

Ukiwa umegunduliwa kwa mara ya kwanza takribani miaka 60 iliyopita, moyo wa bandia wa wakati huo uliwawezesha wagonjwa waliokuwa wakisubiri kupata mtu atakayejitolea kupatikana na uliweza kumsaidia mgonjwa kwa muda tu. Ugunduzi huu mpya, unaweza kutoa suluhisho la kudumu kwa kuwa moyo huo unalenga kumwezesha mgonjwa kuishi maisha yake yote.

Historia inaonyesha kuwa, kipindi kirefu ambacho mgonjwa ameweza kuishi kwa msaada wa teknalojia ya moyo wa bandia uliojulikana kitaalamu SynCardia temporary TAH ni miaka minne.

Katika kile ambacho kinaelezwa kama hatua nzuri ya ugunduzi, Kampuni inayohusika na matatizo ya moyo ya nchini Marekani inayojulikana kama SynCardia Systems Inc inaendesha utafiti na kufanya uchambuzi wa kina kuona kama TAH inaweza kuwa suluhisho la kudumu kwa wagonjwa wanaohitaji kubadilishiwa moyo na kushindwa kuupata kwa wakati kutokana na kuongezeka kwa mahitaji.

“Mwishoni mwa miaka ya 1960 wakati wagonjwa walipoanza kuwekewa mioyo mipya kutoka kwa binadamu wengine, upatikanaji wa kiungo hicho muhimu kwa maisha ya binadamu ulikuwa mkubwa. Upatikanaji wake ulikuwa mkubwa kuliko mahitaji lakini kwa sasa mahitaji yameongezeka zaidi na upatikanaji umepungua,” anasema Danald Isaacs ambaye ni Makamu wa Rais wa SynCardia, akiliambia Shirika la Habari la Fox.com.

Idara ya Afya na Huduma za Binadamu ya Marekani inakadiria kuwa watu 4,000 husubiria kupata moyo mpya ili waweze kuendelea kuishi kila siku wakati mioyo 2,300 ikiwa inatolewa.

Ugonjwa wa moyo ni chanzo namba moja cha vifo nchini Marekani ukigharimu maisha ya watu 611,000 mwaka 2015, hii ni kwa mujibu wa Kitua cha Kupambana na Kuzuia Magonjwa cha nchi hiyo (CDC)

Wakati wa kumwekea mgonjwa moyo wa bandia au TAH, daktari huondoa kwa njia ya upasuaji ventrikali ya kulia pamoja na valvu nne kama ambavyo hufanyika wakati mgonjwa akiwekewa moyo ambao hutolewa na binadamu mwingine ambapo huwekwa wa bandia badala yake.

“Asilimia 96 ya mfumo wa kuweka moyo bandia ni ule wa SynCardia Temporary TAH ambao hutoa suluhisho la muda tu,” anasema Isaacs. Takwimu za SynCardia zinaonyesha kuwa wagonjwa 1,123 wamewekewa mfumo huo ambao ni modeli 70cc.

John Beckingham, mwenye umri wa miaka 58 ambaye ni mhandisi mstaafu anayeishi katika eneo la Rochester jijini New York alifanyiwa upasuaji uliofanikisha kuwekewa moyo mpya katika hospitali ya Cleverland, Oktoba mwaka 2015 baada ya kukaa miezi sita kwenye foleni ya kusubiria. Wakati akisubiria alikuwa akitumia mashine maalumu ambayo ilikuwa ikitumia betri  na ambayo ufanisi wake haukuwa sawa na teknalojia hii mpya.

DR. MAGUFULI ATUNUKU KAMISHENI KWA MAOFISA WA JWTZ

Dr. Rais John Pombe Magufuli, ametunuku kamisheni kwa maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika vyeo  vya Luteni Usu.

Hafla ya kutunuku kamisheni hizo imefanyika leo Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo miongoni mwao wanaume ni  143 na wanawake ni 22.

Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli, Meja Jenerali  Masao, akizungumza katika hafla hiyo amesema wahitimu wa mafunzo hayo ni pamoja na maofisa 15 kutoka mataifa mengine.

MWANAMKE ASIMULIA ALIVYOBAKWA NA ASKARI MSUMBIJI

Wakati Serikali ikiahidi kufanya uchunguzi wa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika kutimua Watanzania nchini Msumbiji, mwanamke mmoja amesema alibakwa na askari watatu kabla ya kuwekwa mahabausu ambako alikaa siku tatu bila kula. 

Mwanamke huyo, aliyejitambulisha kwa jina la Halima (si jina lake halisi) ni mmoja kati ya zaidi ya Watanzania 180 ambao wamekuwa wakitimuliwa nchini Msumbiji tangu mwanzoni mwa wiki na wengi wakidai wana hati halali za kuishi nchi hiyo jirani na wengine kulalamikia vitendo vya ukiukwaji haki wakati wa utekelezaji wa operesheni hiyo. 

Tayari Serikali imesema kuwa itafanya uchunguzi wa madai hayo, ambayo yanaweza kuharibu uhusiano wa muda mrefu wa Tanzania na Msumbiji. 

Halima anasema walianza kufukuzwa usiku wa Jumamosi ya Februari 11, muda ambao askari hao waliutumia kumfanyia kitendo hicho. 

Halima anasema kuwa alisikia watu wakivunja geti la nyumba waliyokuwa wakiishi na kudhania ni majambazi, kumbe walikuwa ni askari ambao waliwalazimisha kutoa nyaraka zao zote za kuishi Msumbiji pamoja na pesa. 

“Niliwasikia wakivunja geti nikamwambia mume wangu watakuwa ni majambazi kumbe askari, mume wangu akajificha chini ya uvungu, lakini wakamtoa na baadaye kututoa ndani na kuanza kutupiga.” 

Anasema baada ya kipigo walilazimishwa kuzoa mali zao kutoka ndani na zikawekwa kwenye gari la polisi na kisha kuwafunga mikono na baadaye kuwapeleka mahabusu. 

“Cha kushangaza tulibebeshwa vitu wenyewe kuweka kwenye gari pasipo kuelezwa sababu baada ya hapo askari akanivuta nyuma ya nyumba na kuniingilia kimwili. Nikajua ni mmoja, lakini waliendelea hadi wakafikia watatu,”alisema. 

“Ninaona aibu walinibaka kwa njia ya kawaida tofauti na taarifa za wengine wanaosema tulibakwa kinyume na maumbile, si kweli. Nawaomba waelewe hatukubakwa kinyume na maumbile kama wanavyosema ilikuwa kawaida.” 

Hata hivyo anaeleza baada ya hapo waliwekwa mahabusu kwa siku tatu pasipo kula, hali iliyowalazimu kunywa maji yaliyokuwa yamewekwa chooni. 

“Tulikaa mahabusu siku tatu, hamna kula wala kunywa, chooni tulienda kwa mtutu tukalazimika kunywa maji ya chooni kwa sababu hakukuwa na jinsi na njaa ilizidi. Kwa hiyo inabidi useme unakwenda chooni ili ukanywe maji,” alisema Halima. 

Kutokana na hali hiyo, Halima anashangazwa na kauli ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Susan Kolimba kwamba waliorudishwa hawakuwa na nyaraka huku kaimu balozi wa Tanzania nchini Msumbiji akiwatangazia wengine kuondoka ndani ya siku tano. 

“Kweli mtu utathubutu vipi kuishi nchi ya watu bila kibali? Hata kaimu balozi na yeye anatukana, kwamba hatujaingia na documents (nyaraka)? Ilibidi atutetee lakini katukana. Mungu atatulipia,” alisema. 

Mwanamke mwingine aliyewekwa mahabusu kabla ya kurudishwa nchini, Mary Makundi anasema askari wa kiume walimwambia awape fedha na alipowajibu kuwa hana, walimpekua na kuzikuta. 

Anasema walizichukua fedha hizo pamoja na simu kabla ya kumpiga na kutaka kumbaka.

“Walivunja mlango wakanikuta. Wakaniambia niwape nyaraka zangu. Nikawapa nikijua wanazikagua tu na kuniacha, lakini cha kushangaza walizichana mbele yangu na kunitaka niwape pesa na simu. Nikawaambia sina wakanipiga na kunikagua hadi sehemu za siri na kuchukua pesa na simu,” alisema Mary. 

“Baada ya hapo walinipiga kwanza kabla ya kunifunga mkono. Askari mmoja akataka kunibaka, nikamwambia kuwa hata kama hawatutaki nchini kwao, hawawezi kuniingilia bila kinga. 

“Nilipoona hali imekuwa mbaya, nilisema wacha nigombane nife kwa silaha, lakini si kubakwa.” 

Mtanzania mwingine Mohamedi Said ni mmoja wa wafanyabiashara walioambiwa waondoke pasipo kuchukua chochote na anadai kuacha mali zake zote pamoja na nyumba aliyojenga. 

“Polisi walikuja ghafla wakatuambia wageni wote tunatakiwa tuondoke. Hapa nina vibali vyote mpaka leseni ya biashara, lakini imebidi niondoke kwa sababu ya usalama wangu,” alisema Said. 

“Hakuna anayejua sababu mpaka sasa. Nimekuja nyumbani kufuatilia haki yangu kwa sababu mpaka kibali cha kujengea ninacho. 

“Mpaka sasa amekuja kaimu balozi kutoka ubalozi wa Tanzania na amesema kwa ripoti aliyopewa ametupa siku tano tuondoke. Hatujui kwanini siku tano. Utahamishaje vitu kwa siku tano au kumtafuta mnunuzi wa nyumba kwa siku tano kwa sababu imenibidi niache duka kubwa na gari,” alisema Said. 

Akizungumzia tukio hilo, mwenyekiti wa Kijiji cha Kilambo kilichopo mpakani na Msumbiji, Mohamed Mkama alisema wananchi wa kijiji chake wamekuwa wakishirikiana na wanakijiji wa vijiji jirani vya Msumbiji, lakini tukio hilo limewashangaza. 

Amesema mara nyingi wamekuwa wakitembeleana na hata wengine kutoka upande wa Msumbiji kuja kutibiwa Tanzania kutokana na ujirani mwema uliopo. 

“Kijiji changu kina vitongoji vitano ambavyo tumekuwa tukishirikiana na kijiji cha upande wa pili kwa muda mrefu na wengine wana vitambulisho vya uraia mwema, lakini tunashangaa kwanini wanarudishwa pasipo kuelezwa sababu,”alisema Mkama. 

Ofisa uhamiaji Mkoa wa Mtwara, Rose Mhagama alisema idadi ya Watanzania waliorudi na kusajiliwa katika mpaka wa Kilambo ni watu 221 hadi kufikia jana mchana. 

KIJANA AZALISHA UMEME KWA MAJI YA MFEREJI PIA AGUNDUA TREKTA KWA INJINI YA PIKIPIKI

Kijana mmoja jina Jackson Mungule mkazi wa Arusha amefanikiwa kuzalisha umeme kwa maji ya mfereji na kuusambaza kwa watu zaidi ya 100. Teknolojia hii ameigundua tokana na tafiti zake ndogo ndogo alizokuwa akizofanya kwa muda mrefu maana yeye kwa muda wote wa maisha yake amekuwa ni mtu mtundu anayejihusisha na mambo ya injini za magari,pikipiki na hata umeme.

Pia anazalisha umeme kwa kutumia kinyesi cha mifugo.
Katika hatua nyingine bwana Mungule amefanikiwa kutengeneza trekta kwa kutumia injini ya pikipiki ambayo inatumia mafuta kidogo hivyo kuweza kuwa mkombozi kwa wakulima.

Ugunduzi huu unaweza kuwa hatua moja muhimu sana katika kuitafuta ile Tanzania ya viwanda ambayo imekuwa ikihubiriwa mara kwa mara na serikali hii ya awamu ya tano ya Dr John Pombe Magufuli,kwani hii inaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa sana katika maendeleo ya shughuli na viwanda na kilimo,mfano kwa sasa ka teknolojia hiyo ya Trekta ikiendelezwa inaweza kuwa msaada mkubwa sana kwa wakulima mkoani Arusha ikibidi hata na Tanzania kwa ujumla kwani inaokoa sana matumizi ya mafuta.

Mgunduzi huyu anaomba serikali imsaidie ili aweze kuongeza ujuzi wake zaidi na kuleta tija kwa taifa hii linaweza kuwa jambo zuri na jema sana hasa katika mapambano ya kuondoa ukosefu wa ajira na hata kuongeza kipato na uchumi wa nchi kwa ujumla.

MAMA ASHIKWA NA POLISI KWA KUFUKUA KABURI LA MWANAE

Wananchi waliojichukulia sheria mikononi wamechoma nyumba ya mama mmoja eneo Mbalizi mkoani hapa, akituhumiwa kufukua maiti ya mwanawe, kuiogesha na kuihifadhi ndani nyumbani kwake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari amethibitisha kushikiliwa kwa mwanamke huyo.
Amesema tukio hilo linalohusishwa na imani za kishirikina limetokea katika Mtaa wa Shigamba, Kata ya Mbalizi. 

Inadaiwa baada ya mtoto wake kufariki dunia, mama huyo aliamini angefufuka siku ya tatu, jambo ambalo halikutokea hivyo aliamua kwenda kufukua kaburi na kumtoa.

LIGI KUU TANZANIA BARA KUPIGWA KESHO

Mechi kali zaidi itakuwa kesho Jumapili kati ya Mwadui watakaokuwa wenyeji wa matajiri wa Juisi, Azam mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex.
Mchezo mgumu zaidi ni wa Mtibwa na JKT Ruvu inayopambana kujinasua na hatari ya kushuka daraja sawa na ule wa Mbao na Majimaji ambazo zote bado hazipo salama katika eneo la kushuka. Ndanda itacheza na African Lyon pia kesho.

MATAIFA 13 YAKUBALIANA KUBORESHA ELIMU AFRIKA

Mataifa 13 za Afrika zikiwamo za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), zimekubaliana kuboresha sekta ya elimu katika nyanja mbalimbali ikiwamo kuweka mifumo bora ya utoaji wa elimu na kutatua changamoto zinazowakabili walimu ikiwamo mishahara na kupanda kwa madaraja.
Akizungumza Dar es Salaam juzi katika kongamano la nchi hizo lililokuwa linajadili elimu jumuishi, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, alisema kwa upande wa Tanzania, Serikali itashirikiana na wizara mbalimbali hapa nchini.
Profesa Ndalichako alisema katika makubaliano hayo, wamepanga kuweka mifumo bora ya utoaji elimu, kuboresha mazingira ya utoaji elimu, kusimamia posho za walimu, mishahara na wale wanaotakiwa kupanda madaraja.
Pia alisema kwa sababu elimu bora huanza kwa mwalimu, hivyo wamekubaliana kuwajengea uwezo wa kufundisha, kuwapa semina elekezi na kubadilishana uzoefu utakaowasaidia kutoa elimu bora.
Alisema ili kuhakikisha kuwa makubaliano yanafanikiwa, wataanzisha mfumo wa kusimamia na kupima utekelezaji wa makubaliano hayo kuanzia elimu ya awali ya umri wa miaka minne hadi sita huku wakiwapima wanafunzi kwa kutumia matokeo ya mitihani ili wale waliofeli zaidi waweze kuangalia namna ya kuwasaidia.
“Katika mfumo huo pia tutaangalia utoaji wa elimu kwa watoto bila ya kujali mazingira yao huku tukiangalia namna ya kuwasaidia watoto wenye vikwazo au matatizo mbalimbali ili waweze kupewa mikakati ya kufaulu,” alisema.
Ndalichako alisema mfumo huo pia wataweza kuangalia utoaji wa elimu ya watu wazima na mtoto wa kike na kuweka mikakati mingine ya uboreshaji wa elimu.
“Tumekubaliana kusimamia kwa ukaribu zaidi mafunzo ya ufundi stadi ili vijana wanaofeli elimu ya juu waweze kujiunga na kupata maarifa zaidi ya elimu ya vitendo, jambo linaloweza kupunguza tatizo la ajira,” alisema.
Kutokana na hali hiyo, alisema wanafunzi watajengewa uwezo wa kujiendeleza pamoja na kusimamia upatikanaji wa takwimu sahihi na kuzifanyia uchambuzi.
Alisema mkakati wa nchi hizo za EAC ikiwamo Somalia, Mauritius na Djibouti ni pamoja na kuhakikisha kuwa wanafunzi wanatapa elimu bora kwa maendeleo ya taifa na nchi hizo jambo linaloweza kuwasaidia kuingia katika soko la ushindani wa ajira ndani na nje ya nchi.

MAKONDA ANAWEZA KUCHUNGUZWA JUU YA UTAJIRI WAKE WA MUDA MFUPI

SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imesema ipo tayari kuhakiki mali za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, endapo watapokea malalamiko kutoka kwa wanaomtilia shaka.
Hivi karibuni wakati akitangaza orodha ya watu wanaotuhumiwa kuuza, kuagiza na kutumia dawa za kulevya,  Makonda alijikuta akiingia katika vita ya maneno na wabunge.
Msingi wa vita yenyewe ni hatua ya baadhi ya wabunge kupinga utaratibu alioutumia Makonda kuwataja kwa majina watuhumiwa hao na hata kwenda mbali zaidi wakimtuhumu na kuhoji alikopata utajiri wa ghafla.
Hatua ya kuhoji mali za Makonda ilichochewa na kauli ya Mkuu huyo wa Mkoa ambaye alionekana kukerwa na ukosoaji wa wabunge hao na hivyo kuwatuhumu wawakilishi hao wa wananchi kulala bungeni na kuitikia kila kitu ndiyoooo.
Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi lililotaka kupata ufafanuzi kwa upande wa sekretarieti hiyo juu ya madai hayo ya utajiri wa Makonda na iwapo aliziorodhesha kama sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya 1995 inavyoelekeza, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa sekretarieti hiyo, Joseph Ishengoma, alisema chombo hicho kipo tayari kufanya uhakiki endapo watapokea malalamiko rasmi kutoka kwa wananchi au wabunge waliosikika hivi karibuni wakizungumzia suala hilo bungeni.
Alisema kinachotakiwa ni kufuata utaratibu ambao ni kupeleka malalamiko kwa sekretarieti hiyo kuomba kufanyika kwa uhakiki wa mali za kiongozi huyo kutokana na tuhuma walizozitoa.
Kauli hiyo ya sekretarieti imekuja ikiwa imepita takribani wiki moja sasa tangu wabunge na Makonda washambuliane kwa maneno.
Miongoni mwa wabunge walioonekana kukerwa na kauli pamoja na utaratibu alioutumia Makonda na hata kutaka naye achunguzwe ni Mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini,  ambaye alikwenda mbali na kutaja mali zinazodaiwa kumilikiwa na Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Akichangia taarifa za Kamati za Bunge  za Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Selasini alisema Makonda amenunua jengo (apartment) lenye thamani ya shilingi milioni 600.
“Makonda amenunua apartment pale Viva Towers kwa shilingi milioni 600, Makonda amempa mke wake gari aina ya Mercedez Benz lenye thamani ya  Dola 250 za Marekani (shilingi milioni 550) kama zawadi ya birthday,” alisema Selasini.
Siku moja kabla ya Selasini kusema hivyo, Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Rushaku (Msukuma), naye aliibuka na tuhuma nyingine nzito dhidi ya Makonda na kutaka vyombo husika vimchunguze.
 “Mheshimiwa Spika, nasimama kwa kanuni ya 68(7) kuhusu jambo lililojitokeza jana (juzi) wakati wa mjadala wa Bunge…naomba mwongozo wako.
“Mimi binafsi naunga mkono jitihada za Rais kukamata wauza dawa za kulevya, lakini dalili ya kwanza ya kuanza kumhisi mtu kama anajishughulisha na biashara ambazo hazieleweki, kwanza ni mwenendo wa mtu yeyote…si mbunge wala si nani.
 “Anatumia Lexus ya petroli ya Sh milioni 400, lakini imekarabatiwa ofisi (yake) ya RC Dar es Salaam kwa zaidi ya Sh milioni 400 bila kufuata utaratibu wa manunuzi wa Serikali.

“Ana ma-V8 na Mwanza amejenga jengo la ghorofa…ni kina nani wanaotakiwa kujadiliwa na kufanyiwa uchunguzi? Na hawa mawaziri tulionao humu kwanini wamepigwa ganzi? Utawala bora, Mambo ya Ndani na Waziri wa Sheria…kwanini mmepigwa ganzi?”
Msukuma pia alihoji anakopata fedha Makonda za kwenda Paris na Marekani na kukaa siku 21 hasa ikizingatiwa kuwa tiketi moja ni Dola za Kimarekani 14,000 huku yeye na mkewe jumla ikiwa ni dola za Kimarekani 28,000.
Kutokana na hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Sekretarieti hiyo, Ishengoma, alisema wabunge hao baada ya kutoa malalamiko ya kutilia shaka mali za Makonda, wanatakiwa kulipia kiasi cha shilingi 1,000 na kisha watapewa faili kwa ajili ya kuangalia na kujiridhisha mali ambazo Makonda alizitaja kwao.
Alisema na hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995.
Alisema kwa kuzingatia Katiba na sheria hiyo, Sekretarieti itakuwa na wajibu wa kupokea hati za tamko rasmi zinazohitajika kutolewa na viongozi wa umma kwa mujibu wa Katiba au sheria nyingine yoyote.
Alisema kifungu cha 18 (b) kinaeleza kuwa; Sekretarieti itapokea malalamiko na taarifa za ukiukwaji wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma kutoka kwa wananchi.
Kifungu cha 18 (c) Sekretarieti itachunguza tuhuma yoyote ya kuvunjwa kwa sheria ya maadili ya viongozi wa umma na viongozi wote wa umma wanaopaswa kuwajibika chini ya sheria hiyo.
Alisema pia sekretarieti katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa vipengele hivyo, itakuwa na mamlaka  ya kupokea na kusikiliza malalamiko yote kuhusu kiongozi yeyote wa umma yawe kwa mdomo au kwa maandishi kutoka kwa si tu wabunge hao bali kwa mwananchi yeyote bila kuuliza majina na anwani za watu waliopeleka malalamiko hayo.
Kwa mujibu  wa sheria ya maadili ya mwaka 1995 (23) (1) endapo mtu mwenye wadhifa wa waziri au wa mkuu wa mkoa amekiuka miiko hiyo malalamiko yanaweza kuwasilishwa kwa rais na mtu yeyote kwa maandishi yaliyotiwa saini, anwani na jina la mlalamikaji.
Zaidi, Ishengoma alisema taarifa ya mali za Makonda pamoja na viongozi wengine ziliwasilishwa katika ofisi yao Desemba 31, mwaka jana kwa mujibu wa sheria.
Alisema pamoja na hayo hatamzuia mtu kupeleka kile anachokijua ili waweze kufanyia kazi.
“Sheria hii yenyewe inampa mtu ‘Comsumption’ kama Kamishna wa Tume ya Maadili ataangalia kama mali zake zina ushahidi na ofisi inaweza kufanya uhakiki wa kupata taarifa sahihi kama alificha hizo mali hapo awali au la na hatua ya kwanza atapewa kubadilisha.
“Na kama Kamishna akiridhia kuwa amedanganya basi atapelekwa katika Baraza la Maadili na anayelalamika  anakuwa ni miongoni mwa mashahidi na kitakachofuata atajitetea na chombo hicho kitatoa mapendekezo,” alisema Ishengoma.

KAMATI YA BUNGE YABAINI KASORO UJENZI NSSF

 Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imeeleza kuthibitisha madudu katika utekelezaji wa mradi wa nyumba za kisasa wa Dege Eco Village Kigamboni ambao  ujenzi wake umesimama.
Mradi huo  ulikuwa unaendeshwa kwa pamoja na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), ambayo inamiliki asilimia 45 za hisa na kampuni ya Azimio Housing Estates (AHEL) inayomiliki asilimia 55.
Jana, mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka amesema kamati hiyo imeikabidhi Ofisi ya Bunge ripoti ambayo pia ina mapendekezo kwa ajili ya hatua zaidi.
Kaboyoka amesema ripoti hiyo imesheheni mambo mengi ambayo alikataa kuyataja akisema wakati ukifika yatatajwa.  “Ifahamike ni madudu sana ambayo yanakera.”
Mradi wa Kigamboni una thamani ya Dola 653,436,675  za Marekani (Sh1.3 trilioni).
Awali, kashfa hiyo iliibuliwa katika ripoti ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2013/14 na gazeti hili kuianika katika habari mfululizo.

RAIS MAGUFULI ATUNUKU NISHANI KWA MAAFISA 165 IKULU DAR LEO

Rais John Magufuli, ametunuku kamisheni kwa maofisa 165 wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika vyeo  vya Luteni Usu hata hivyo pamoja na hao wapo pia Maafisa wengine wachache toka nchi za Rwanda,Uganda na Kenya wapatao 15 nao pia kwa pamoja wametunukiwa nishani ya Luteni Usu.
Hafla ya kutunuku kamisheni hizo imefanyika leo Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo miongoni mwao wanaume ni  143 na wanawake ni 22.
Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli, Meja Jenerali Paul Masao, akizungumza katika hafla hiyo alisema wahitimu wa mafunzo hayo ni pamoja na maofisa 15 kutoka mataifa mengine.

SERIKALI YAJIPANGA KUZUIA UVUTAJI SIGARA OVYO

Wizara ya Afya ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema ipo katika hatua za mwisho za kutayarisha mwongozo wa kupiga marufuku matumizi ya uvutaji wa sigara hadharani ili kudhibiti maradhi yasiyoambukiza yanayotokana na sigara.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo wakati akitoa ufafanuzi kuhusu uvutaji wa sigara hadharani katika sehemu za mkusanyiko na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi.

Alisema tayari Wizara ya Afya imewasilisha muswada wa kulinda afya ya jamii ambao moja ya kazi yake kubwa ni kupambana na matumizi ya sigara katika jamii na sehemu za mkusanyiko.

Akifafanua zaidi, alisema utafiti uliofanywa kuhusu maradhi yasiyoambukiza unaonesha kwamba upo kwa asilimia 38 ambayo yanahusishwa na uvutaji wa sigara.

Kombo alisema mwongozo huo ukikamilika utaletwa mbele ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na wajumbe kutoa maoni yao kabla ya kufanya kazi na kuwa sheria inayotakiwa kutekelezwa na kusimamiwa.

Alisema yapo matumizi mabaya ya uvutaji wa sigara hadharani ikiwemo sehemu za mikusanyiko ya watu kama hospitalini na sehemu za kusubiri usafiri wa abiria na kusababisha madhara makubwa ambayo hayaonekani kwa mara moja.

YUSUPH MANJI ALAZWA TENA HOSPITALI

Baada  ya kupata dhamana ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu juzi, mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji, amelazwa tena kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyoko katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na Ofisa Uhusiano wa Taasisi hiyo jana, Anna Nkinda, Manji alifikishwa hospitalini hapo juzi jioni ikiwa ni muda mfupi baada ya kupata dhamana dhidi ya kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya heroin inayomkabili.

“Ni kweli Manji yupo hapa, aliletwa jana jioni (juzi) kwa matibabu ambapo hadi leo (jana) ninavyoongea na wewe bado yupo hapa amelazwa anaendelea na matibabu kama kawaida,” alisema Anna.

Hii ni mara ya pili kwa Manji ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu, kulazwa kwenye taasisi hiyo.

Mara ya kwanza ilikuwa ni Februari 12, mwaka huu alipolazwa hapo akitokea katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, alipokuwa ameshikiliwa tangu Februari tisa akifanyiwa mahojiano.

Mfanyabiashara huyo alifika mwenyewe kwenye kituo hicho cha polisi kutokana na wito uliotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, aliyetaja majina 65 ya watu aliodai wanajihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Mbali na Manji, baadhi ya watu wengine waliotajwa na Makonda na kutakiwa kufika kituoni hapo ni Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, Mbunge wa zamani wa Kinondoni, Idd Azzan ambao tayari wamehojiwa polisi huku Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, akiwa bado hajahojiwa licha ya kutajwa kwenye orodha hiyo.

Juzi Alhamisi, Manji alifikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambapo shauri lake lilisikilizwa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Cyprian Mkeha.

Karani wa mahakama hiyo, Sarah Mulokozi, alimsomea mshtakiwa shtaka lake ambapo alidai kuwa kati ya Februari 6 na 9, mwaka huu eneo la Upanga Sea View jijini Dar es Salaam, Manji alitumia dawa za kulevya aina ya heroin.

Mtuhumiwa huyo alikana shtaka hilo na Mkurugenzi wa Mashtaka Msaidizi (ADPP), Osward Tibabyekomya, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuiomba Mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.

Upande wa mawakili wa utetezi ambao ni Alex Mgongolwa na Hudson Ndusyepo, waliiomba Mahakama kumpa mshtakiwa dhamana  kwa sababu ya mashtaka yanayomkabili yanadhaminika.

Hakimu Mkeha alisema mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana kwa kutakiwa kusaini hati ya dhamana ya Sh milioni 10 pamoja na mdhamini mmoja wa kuaminika ambapo Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga, Charles Mkwasa, alimdhamini Manji, ambaye aliachiwa kwa dhamana hadi Machi 16.

Mara baada ya kupata dhamana, Manji aliondoka mahakamani hapo saa 9:40 akiwa kwenye gari yenye namba T670 BBX aina ya Hummer.

BARAZA LA KUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA LAZINDULIWA

Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa amezindua Baraza la kudhibiti madawa ya kulevya. Akizungumza na  Mawaziri na Wajumbe wa Baraza la Taifa la Udhibiti wa Dawa za Kulevya Nchini  wakati akifungua kikao cha Baraza hilo leo Jijini Dar es Salaam ameonya vikali wajumbe hao kutojihusisha na rushwa.

MWALIMU MKUU AVULIWA MADARAKA KWA KUSHINDWA KUSIMAMIA UTOAJI WA ADHABU

Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Uyowa Tabora amevuliwa madaraka ya kuwa mwalimu mkuu na kuwa mwalimu wa kawaida kwa kushidwa kusimamia utoaji wa adhabu shulenikwake.

Jumanne mkuu huyo hakuwepo shuleni alienda kwenye semina wilayani na hapo Shuleni kulikuwa na ukaguzi wa usafi kwa wanafunzi na ikabainika watoto wengi wakakutwa wachafu na wamevaa nguo kwa kujaladia(yaani nguo mbili mbili).

 Walimu wakaamuru wakazitoe hizo nguo walizo jaladia na watoto hao wakaadhibiwa na walimu ghafra ikaibuka tafrani toka kwa wazazi wakaja juu karibia kijiji kizima wanataka kuwapiga walimu kwa kuwapiga watoto wao kitendo kile  kilikuwa kizito ikabidi kwa usalama wa wa Walimu wakachukuliwa kwenda kulala kituo cha polisi Ulyankulu.

Jana timu ya Halmashauri walifika hapo shuleni wakiongozwa na Afisa Elimu Msingi, baada ya uchungunzi kukamilika wakamvua madaraka mkuu wa shule hiyo na kuondoka na majina kadhaa ya walimu,mpaka sasa haijafahamika ni adhabu gani zaidi watapewa walimu hao dhidi ya tukio hilo.

MKURUGENZI AVUNJA KIKAO CHA MADIWANI MERU

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Meru Bwana Christopher Kazeri kwa masikitiko makubwa na kwa mshangao mkubwa jana alivunja kikao na kuwaamuru wataalam watoke nje ya ukumbi wa halmashauri.

Sababu kubwa ni kushindwa kujibu maswali ya waheshimiwa Madiwani kuhusu kuvurugwa kwa bajeti ya halmashauri na kuacha vipaumbele vya halmashauri na kuingiza vitu ambavyo siyo kipaumbele cha halmashauri kwa sasa.

Kwa mfano amefoji na kuingiza kwenye bajeti ununuzi wa gari la mkurugenzi, ujenzi wa nyumba za wafanyakazi, na ununuzi wa wa pikipiki za watendaji. Hivi siyo vipaumbele vya halmashauri kwa sasa. Sasa alivyobanwa na maswali kuhusu haya ndipo alipoamua kukimbia kikao na kuwaamuru watendaji watoke nje.

Hali hiyo ilipelekea kikao kuvurugika na wajumbe wote kutawanyika na baadhii kukaa makundi makundi wakijadili sintofahamu juu ya Mkurugenzi huyo.

HATUA ZICHUKULIWE KUOKOA MAISHA SOMALIA


Wakati ukame ukiighubika Somalia shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na lile la mpango wa chakula duniani WFP wameonya kwamba msaada pekee mkubwa ndio utalisaidia taifa hilo kuepuka kutumbukia katika zahma nyingine ya kibinadamu.

Taarifa ya pamoja ya mashirika hayo imesema ukame uliolikumba eneo la kaskazini mwa nchi hiyo mwaka jana sasa umesambaa Somalia nzima na kutishia mamilioni ya watu ambao tayari wameathirika na miongo kadhaa ya vita.

Watu milioni 6.2 ama hawana uhakika wa chakula au wanahitaji msaada na inatarajiwa watoto 944,000 watakabiliwa na utapia mlo mwaka huu.Laurent Bukera ni mkurugenzi wa WFP nchini Somalia

MASHABIKI YANGA WAONYWA MECHI YA LEO DHIDI YA NGAYA FC


Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania mashabiki wote wa Yanga waliojiandaa kwenda na mabango ya kukashifu serikali,hili limeelezwa linaweza kutokea kwani Shirikisho lina taarifa hizo.

Mashabiki hao wamejiandaa kufanya hivyo kutokana na mwenyekiti wao Yusuph Manji kushikiliwa na Polisi baadae kupelekwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia madawa ya kulevya.

Shirikisho limesema vitendo hivyo vikifanyika vinaweza kuleta uvunjifu wa amani na hata kupelekea uharibifu wa uwanja kama uliofanyika kipindi na katibu mkuu akaonya kuwa safari hii tukio kama hilo likitokea inaweza kuwaamusha zaidi na kuifungia timu hiyo kutokuutumia Uwanja wa taifa moja kwa moja kwani itakuwa ni dharau na utomvu wa nidhamu uliopitiliza kwa serikali,pia akakumbushia kauli iliyowahi kutolewa na serikali dhidi ya timu zinazoharibu miundombinu ya viwanja yeye Rais hawezi kwenda kuangalia mechi kama hizo ni bora akaangalie mechi za mchangani.

MAGAZETI YA LEO 18/2/2017
























MGANGA WA KIENYEJI AMBAKA MGONJWA WA AKILI MWANZA

Mganga mmoja wa kienyeji huko jijini anashikiliwa juzi baada ya kumuingilia kimwili mgonjwa wa akili aliyekuwa anamtibu nyumbani kwake,mganga huyo wa kienyeji amekuwa na utaratibu wa kuwatibu wagonjwa mbalimbali.

Mgonjwa huyo aliletwa nyumbani kwa mganga huyo baada ya ndugu zake kumsafirisha kutoka nyumbani Kahama mkoani Shinyanga kwani sifa za mganga huyo kuhusu tiba zilisikika maeneo mengi. Ndugu wa mgonjwa huyo walimleta na kurudi nyumbani Kahama ili waweze kwenda kujipanga namna ya kupata fedha za kulipia gharama za matibabu pia hata chakula lakini baada ya kurudi ndugu hao kwa mganga huyo aliwaeleza juu ya kitendo alichofanyiwa na mganga huyo na kwenda kuripoti Polisi ambapo mgonjwa alienda kupimwa hospitali na kithibitisha kuwa alifanyiwa kitendo hicho.

Watu wengi hasa maeneo ya mikoa ya Kanda ya ziwa wamekuwa na utaratibu wa kupeleka wagonjwa wao katika tiba mbadala kwa ajili ya kutibiwa wakiamini kuwa maradhi mengi yanaletwa na kurogwa. Dhana hizi zimekuwa zikiendelea miaka hadi miaka na kupelekea kuongezeka imani za kuua wazee kwa mapanga.

Mganga huyo anaendelea kushikiliwa na Polisi na atafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika.

Propellerads