Ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, ameuawa nchini Malaysia, kwa mujibu wa Korea Kusini.
Kim Jong-nam mwenye umri wa miaka 45, anaripotiwa kulengwa kwenye uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur.
Kim Jong-nam mwenye umri wa miaka 45, anaripotiwa kulengwa kwenye uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur.
Polisi nchini Malaysia wamethibitisha kwa shirika la Reuters kuwa mwanamume raia wa Korea Kaskazini ambaye alifariki wakati akipelekwa hospitalini kutoka uwanja wa ndege ni Bwana Kim.
Kwa mujibu wa ripoti ya televisheni ya Chosum nchini Korea Kusini, Bwana Kim aliwekewa sumu akiwa uwanja wa ndege na wanawake wawili wanaoaminiwa kuwa maajenti wa Korea Kaskazini.






0 comments:
Post a Comment