"Majeshi yamekomboa maeneo yote makubwa ya mafuta", katika mkoa wa kaskazini mwa Libya, amesema Khalifa al-Abidi, msemaji wa vikosi vinavyomtii Khalifa Haftar. Mkuu wa kikosi cha ulinzi kwenye maeneo hayo ya mafuta amethibitisha kutekwa kwa maeneo ya Ras Lanuf na al-Sedra.
Vikosi vya Libya vyatangaza kudhibiti robo ya mji wa Benghazi
Mwishoni mwa mwezi Januari mwaka huu vikosi vya mashariki mwa Libya vilitangaza kudhibiti karibu eneo nzima lililokua likikabiliwa na mapambano ya muda mrefu katika mji wa Benghazi.
Nchi ya Libya inakabiliwa na mapigano kati ya majeshi ya serikali ya Umoja inayotambuliwa na jumuiya ya kimataifa na makundi ya waasi, ikiwa ni pamoja na vikosi vinavyomtii Marshal Khalifa Haftar.






0 comments:
Post a Comment