Ripoti hiyo inayoituhumu Israel kwa ubaguzi wa rangi dhidi ya Wapalestina,imechapishwa jumatano wiki hii na umoja huo unaoundwa na nchi 18 za Kiarabu.
Bi Khalaf,amewaambia waandishi wa habari mjini Beirut,Lebanon,jana,kuwa,ilikuwa inatarajiwa kuwa Israe na washirika wake watamshinikza Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa,kutojihusisha na ripoti hiyo na kumtaka aiondoe katika website ya Umoja wa Mataifa.
Katika hatua nyingine,Mwanamama,huyo,amesema,jana asubuhi,katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,amemuamuru kuiondoa ripoti hiyo na kwamba hakuona sababu ya kuiondoa hivyo kuandika barua ya kujiuzulu wadhifa wake.






0 comments:
Post a Comment