Shujaa aliyepinga ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini Winnie Madikizela-Mandela, amelazwa hospitalii kwa kile kinachotajwa kuwa kufanyiwa uchunguzi wa kiafya.
Familia yake inasema kuwa alipelekwa hospitali ya Milpark mjini Johannesburg.
Mwezi Disemba mwaka uliopita, Bi Madikizela-Mandela alilazwa hospitali hiyo lakini kile kilichosababisha alazwe hakikutajwa.
Msemaji wake Victor Dlamini, alimwambia mwandishi kuwa alikuwa ameenda kufanyiwa uchunguzi wa kawaida lakini madaktari wakaamua kumlaza.
Bi Madikizela-Mandela alikuwa mke wa Nelson Mandela, na alikuwa mwanamke wa kwanza mweusi kusajiliwa kama mhudumu wa kijamii nchini Afrika Kusini.
Thursday, 9 March 2017
Winnie Mandela alazwa Hospitali Afrika kusini
Unknown
No comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)





0 comments:
Post a Comment