Propellerads
Propellerads
Propellerads
Daily Updates!

We share informations with you

Propellerads

Friday, 10 March 2017

Masha,Lissu wataka wawemo kesi ya Tanganyika Law Society


Wanasheria wawili wa jijini Dar es Salaam, Tundu Lissu na Lawrence Masha wamesema wataiomba mahakama kuwajumuisha kama wadaiwa katika kesi za kupinga uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) walizodai zimefunguliwa jijini Dar es Salaam na Dodoma.

Lissu, ambaye ni mbunge wa Iramba na mwanasheria wa Chadema, na Masha (mwanachama wa Chadema na waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani) wamedai kuwa kesi hizo mbili zimefunguliwa Mahakama Kuu na Godfrey Wasonga mjini Dodoma na Onesmo Mpinzile jijini Dar es Salaam, wakitaka uchaguzi huo uzuiliwe.

Mawakili hao wamewahi kupambana katika kesi mbili tofauti zilizohusu vyama vya CCM na Chadema.

Wasonga aliwahi kupambana na Lissu katika kesi iliyofunguliwa na wanachama wawili wa CCM mjini Dodoma waliopinga ushindi wa mbunge huyo wa Singida Mashariki katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2010, wakati Mpinzile alipambana na mwanasheria huyo wa Chadema aliyekuwa akimtetea mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali ambaye amehukumiwa miezi sita jela.

Hata hivyo, Wasonga alisema jana kuwa hajafungua kesi ila anakusudia kufanya hivyo.

Hatua ya Lissu, ambaye ni mwanasheria mkuu wa Chadema, kuchukua fomu ya kuwania urais wa TLS akisema imechagizwa na kauli ya Rais John Magufuli dhidi ya mawakili, ilibadili upepo wa uchaguzi huo na kumlazimu Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe kuuzungumzia akisema Serikali haitavumilia kuona chama hicho kinajiingiza katika siasa.

TLS imekuwa ikafanya uchaguzi kila mwaka, lakini umekuwa hauna harakati kubwa kama ulivyo wa mwaka huu. Tayari TLS imepitisha wagombea urais, wakiwamo Lissu na Masha.

Mbali na kuwa mawakili, Masha na Lissu, ambao wote wanawania urais, ni wanachama wa Chadema, jambo linaloonekana kuchochea mjadala wa siasa kuingia katika chama hicho.

Lakini, mgombea mwingine, Godwin Mussa Mwapongo, pia ni kada wa CCM aliyechukua fomu za kuwania kupitishwa na chama hicho kugombea urais mwaka 2015 ingawa hakufanikiwa. Mgombea mwingine ni Victoria Mandari.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Lissu alisema wamepata wasiwasi kuwa huenda kukawa na njama za washtakiwa katika kesi hiyo, ambao ni TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kutojitetea vya kutosha na hivyo kukubali mashtaka ili uchaguzi huo uzuiwe.

Alisema ili hali hiyo isijitokeze, wataiomba masjala ya Mahakama Kuu iliyopo Dar es Salaam, iwaunganishe katika kesi hizo kama wadaiwa.

“Uchaguzi ukizuiwa, maslahi yetu sisi tunaogombea yatakuwa yamevurugwa kwelikweli. Kwa sababu hiyo na kwa mujibu wa taratibu zinazoruhusiwa kisheria, sisi ambao tunagombea na wapigakura wanaotaka, tutapeleka maombi haraka ili tuunganishwe kwenye kesi zile kama wadaiwa,” alisema Lissu.

“Tutanunua ile kesi, kusije kukawa na njama za uongozi wa sasa wa TLS kuendelea kuongoza baada ya muda wao wa kikatiba kuisha na kusije kukawa na njama ya kuzuia uchaguzi na wale ambao wanataka kuvuruga TLS wakafanikiwa.”

Lissu alisema lengo jingine ni kutaka masuala ya uchaguzi huo yasije yakaamuliwa nyuma ya migongo yao au juu ya vichwa vyao na hivyo wanataka kupata fursa kamili ya kuiambia mahakama kwanini maombi hayo ya kuzuia uchaguzi hayana msingi wowote.

Aliongeza kuwa mawakili hao walioamua kuweka mapingamizi ni wanachama wa TLS na walikuwa na nafasi ya kuweka mapingamizi baada ya kamati ya uteuzi kutangaza majina ya wagombea.

“Kulikuwa na kipindi cha karibu wiki mbili cha kuweka mapingamizi dhidi ya wagombea walioteuliwa, fursa hiyo mwisho wake ilikuwa Machi 15 mwaka huu, lakini hakuna hata mmoja wao aliyeweka mapingamizi hayo. Itabidi tuwahoji,” alisema.

Kwa upande wake, Masha alisema hakuna mtu hata mmoja kati ya wagombea wote wa urais aliyeamua kuingia na kugombea kwa sababu za kisiasa.

Masha alisema licha ya kuwa hana nafasi ya uongozi Chadema, ni mwanachama aliyekuwa wa kwanza kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya urais kabla Lissu hajachukua fomu hiyo.

Alisema kama kungekuwa na mbinu za kisiasa, yeye na Lissu wasingechukua fomu ya kuwania nafasi moja.

“Lissu alikuja kuchukua fomu baada ya muda wa kus

0 comments:

Post a Comment

Propellerads