Maafisa wa Marekani wamepinga pendekezo kwamba Korea Kaskazini itasitisha majaribio ya makombora yake na yale ya Kinyuklia iwapo Marekani itasitisha vitendo vyake katika eneo hilo.
Idara ya maswala ya kigeni nchini humo imesema kuwa mpango huo hautasaidia huku balozi wa Umoja wa Mataifa akisema kuwa Korea Kaskazini haifikirii.
Pendekezo hilo la China linajiri baada ya Korea kaskazini kufanya majaribio ya makombora yake manne ikiwa ni ukiukaji wa vikwazo vya kimataifa.
Wakati huohuo, Marekani imeanza kupeleka mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora nchini Korea Kusini.
Pia inaendela na mazoezi ya pamoja na wanajeshi wa Korea Kusini hatua inayokasirisha Korea kaskazini.
Thursday, 9 March 2017
Marekani yapinga pendekezo la China kuhusu Korea Kaskazini
Unknown
No comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)





0 comments:
Post a Comment