Propellerads
Propellerads
Propellerads
Daily Updates!

We share informations with you

Propellerads

Tuesday, 14 March 2017

Basi lagongana na gari dogo Shinyanga


Basi la RUKSA CLASSIC lenye namba za usajiri T636AWC likitoka jijini Mwanza kwenda mkoani Kigoma limegongana uso kwa uso na gari dogo lenye namba za usajiri T 210 DJJ katika kijiji cha Nhelegani mkabala na chuo cha Ushirika Moshi kambi ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.

Chanzo cha ajali hiyo iliyotokea majira ya nne asubuhi inaelezwa kuwa ni uzembe wa dereva wa gari ndogo ambaye hakuwa na utulivu barabarani na kujikuta yupo upande usio sahihi na kusababisha ajali.

Hata hivyo hakuna mtu aliyepoteza maisha ingawa dereva wa gari dogo na abiria wake mmoja, wameumia na kukimbizwa katika hospitali ya rufaa mkoa wa Shinyanga.Mwandishi wa habari hii alifika eneo la tukio mapema kabisa.

0 comments:

Post a Comment

Propellerads