Kampuni kubwa za madini ya dhahabu zimepewa wiki sita kujiandikisha katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ametoa agizo hilo alipotembelea mgodi wa RZ.
Mwishoni mwa Januari watu 15 katika mgodi huo walifukiwa na kifusi cha udongo.
Amewataka makamishna wa madini kote nchini kufuatilia na kuhakikisha kampuni zote zimejiandikisha kwenye soko la hisa na kwamba, lengo ni kutaka Watanzania wanufaike na uwapo wa rasilimali hiyo.





0 comments:
Post a Comment