Propellerads
Propellerads
Propellerads
Daily Updates!

We share informations with you

Propellerads

Tuesday, 21 February 2017

WANAFUNZI WAUAWA GUINEA KWA RISASI

Takriban watu watano wameuawa nchini Guinea wakati vikosi vya usalama vilipopambana na wanafunzi waliokuwa wakiandana wakitaka mgomo wa walimu kumalizika.
Wanafunzi walijitokeza kwa wingi na kwa hasira wakaanza kuwatupia polisi mawe.
Maafisa walithibitisha vifo hivyo na kuwalaumu waandalizi wa maandamano kwa kupanga kile kilichotajwa kuwa maandamano haramu.
Mfanyakazi mmoja wa hospitali aliliambia shirika la AFP kuwa waliouawa walipigwa risasi kwa karibu na polisi wa kuzima maandamano.
Takriban watu 30 walijeruhiwa wakiwemo maafisa wa vikosi vya usalama.
Waalimu nchini Guina wamekuwa kwenye mgomo wakilalamikia mishahara duni.

0 comments:

Post a Comment

Propellerads