Propellerads
Propellerads
Propellerads
Daily Updates!

We share informations with you

Propellerads

Saturday, 18 February 2017

HISTORIA:WAUWAJI WALITUMIA CHAI,MIAVULI NA SUMU KUWAANGAMIZA WAPINZANI

Hakuna jambo jipya kuhusu mauaji ya mtu maarufu.
Ni miongoni mwa njia zilizotumika kuwaondoa ulimwenguni watu waliokuwa na uwezo mwingi am watu hatari.

Lakini wauaji wengine walitumia njia za moja kwa moja kwa mfano Julius Caesar alidungwa kisu hadi kufa huku Abraham Lincoln akipigwa risasi.
Hivi sasa kuna uvumi kwamba kifo cha Kim Jong nam -ndugu wa kambo wa rais wa Korea kaskazini Kim Jong Un huenda pia aliuawa.
Iwapo hilo limethibitishwa kuwa kweli, basi uvumi umezuka kwamba wanawake wawili waliomuwekea kitambaa cha kujifutia chenye sumu katika mdomo wake alipokuwa akitembea katika uwanja wa ndege mauaji yake yanaorodhshwa miongoni mwa watu wachache waliouawa kupitia njia zisizo za kawaida

Kifo cha Alexander Litvinenko's kinadaiwa kuwa cha mtu maarufu katika miaka ya hivi karibuni.
Jasusi huyo wa Urusi alianza kuugua mnamo tarehe 1 mwezi Novemba 2006, saa chache tu baada ya kunywa chai katika hoteli ya Millenium huko Mayfair pamoja na majasusi wenzake wawili.

Baada ya kifo chake majasusi hao ndio waliokuwa washukiwa wakuu katika kifo chake.

Alexander Litvinenko alitiliwa chai iliowekwa sumu ya Polonium 210
Wakati bwana Litvinenko alipolazwa hospitalini mnamo tarehe 3 mwezi Novemba aliwaambia madaktari amepewa sumu.
Baadaye, alimtaja rais Vladmir Putin akisema ''ndiye aliyesababisha kifo chake''.
Wakati huohuo nywele zake zilianza kuanguka huku viungo vyake vya mwilini vikishindwa kufanya kazi-huku madaktari katika hosptali ya chuo kikuu cha London nchini Uingereza wakishindwa kupata chanzo.

Baadaye ilibainika ni nini kilichomuua kwani wanasayansi bingwa wa Uingereza wanaofanya utafiti wa zana za nyuklia huko Aldermaston walifanikiwa kugundua kwamba tembe ya polonium 210 iliotumika katika bomu la kwanza la nyuklia ndio chanzo cha mauaji hayo.
Hakuna kitu madaktari walichoweza kufanya.
Huenda rais Putin 'aliidhinisha' mauaji ya Jasusi
Bwana Litvinenko aliambia BBC Urusi kwamba alikuwa akichunguza mauaji ya mwanahabari Anna Politkovskaya mwezi uliopita wakati aliposhambuliwa, Alifariki tarehe 23 mwezi Novemba.

Mwavuli uliowekwa sumu.

Raia wa Bulgaria Georgi Markov alikuwa akisubiri kupanda basi mnamo tarehe 7 mwezi Septemba wakati alipohisi amedungwa kisu katika paja lake.
Bwana Markov mwenye umri wa miaka 49 aliangalia nyuma na kumuona mtu ambaye alikuwa amebeba mwavuli akikimbia na kupanda teksi.
Ni baadaye alipokamilisha kazi yake ya huduma ya BBC nchini Bulgaria aliporudi nyumbani na kuanza kuugua.
Bwana Markov ambaye alikuwa mpinzani wa serikali ya kikomyunisti ya Bulgaria alifariki miaka minne baadaye.

Maafisa baadaye waligundua kwamba aliwekewa sumu ya ricin ambayo ilidaiwa kutiwa katika mwavuli huo.
Hakuna mtu aliyeshtakiwa kwa mauaji yake ikiwa ni mabaya zaidi katika vita baridi, lakini Bwana Markov alisema kuwa anaamini kwamba majasusi wa Urusi KGB walihusika katika shambulio lake.

Dubu aliyebeba shoka.

Jörg Jenatsch alikuwa muhubiri ambaye alibadilika na kuwa mwanasiasa maarufu katika vita vya miaka 30 nchini Switzerland.
Lakini licha ya mafanikio yake yote ni kifo chake mwaka 1639 katika nyumba moja ya kulala huko Chur ambacho kitakumbukwa sana.

Mwanasiasa huyo aliuawa na mtu aliyekuwa amevalia kama dubu mwaka 1639.
Bwana Jenatsch, ambaye alikuwa amesifika kwa huduma yake alikuwa katika sherehe wakati kundi moja la watu lilipowasili na kutaka kujiunga nao.
Kiongozi wa kundi hilo alikuwa amevaa kama dubu.
Kundi hilo liliruhusiwa kuingia na dubu huyo ambaye utambulisho wake haukujulikana kabla ya kumkata bwana Jenatsch hadi kufa kwa kutumia shoka.
Inadaiwa kuwa shoka lililotumiwa ndio hilo hilo alilotumia kumuua mpinzani wake.

Chuma cha moto

Zaidi ya miaka 700 huenda imepita tangu mfalme Edward wa pili alipouawa kati mji wa Gloucestershire, lakini bado tunaweza kukumbuka.
Tunachojua ni kwamba mfalme Edward wa pili alikamatwa na kulazimishwa kuwachia ufalme kwa niaba ya mwanawe ambaye alikuwa Edward wa tatu ba

0 comments:

Post a Comment

Propellerads